TANTRADE YASHIRIKI MKUTANO WA MAANDALIZI YA EXPO 2023 DOHA


10 Septemba, 2023.

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeshiriki mkutano wa mwisho wa maandalizi ya Expo 2023 Doha unaofanyika tarehe 10-11 Septemba, 2023, Doha, Qatar.

Mkutano huo umeshirikisha Makamishna wakuu wa Nchi 56 Duniani zinazoshiriki Maonesho ya Kilimo cha Mboga Mboga yanayojulikana kama Doha Horticultural Expo ukiwa ni muendelezo wa matayarisho hayo ambapo Timu ya Expo iliwasilisha hatua za matayarisho kwa makamishna hao ili kurahisisha ushiriki wao katika maonesho yanayotarajiwa kuanza tarehe 2 Octoba, 2023 hadi 28 Machi 2024.
Kwa upande wa Tanzania, mkutano umewakilishwa na Bw.Tahir M.Ahmed na Bi. Mwanaidi K. Chilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa Banda la Tanzania, Bi. Latifa M. Khamis, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade.

TANTRADE KUSHIRIKI KATIKA UFUNGUZI WA MAFUNZO YA UJASILIAMALI KWA WANAWAKE


DAR ES SALAAM.
12 SEPTEMBA, 2023

Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania (TanTrade) kushiriki na wafanyabiashara katika  ufunguzi wa mafunzo na kufanya mdahalo kuhusu   Ujasiliamali katika ukumbi wa Kibada Garden Kigamboni- Dar es salaam tarehe 12 Septemba, 2023.

Ambapo, Afisa wa TanTrade Bi.Lulu Masanje amesema Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania inatoa mafunzo juu ya kujikwamua kibiashara ndani na nje ya nchi ambapo jukumu la kwanza ni kutoa taarifa mbalimbali za biashara ambazo zinampa fursa mfanyabiashara kufahamu kuhusu takwimu ambazo  bidhaa zinauzwa sana na kuongeza soko kwa wingi zaidi na itamsaidia mfanyabiashara kufanya maamuzi sahihi kwaajili ya kujikwamua kiuchumi.

Vilevile, TanTrade inatoa fursa za masoko, mabanda ya maonyesho na usafirishaji wa bidhaa kwenda nchi mbalimbali ambapo fursa hizi   zitachangia katika kuongeza uchumi binafsi na nchi kwa ujumla. Kadhalika, kutambua takwimu za bidhaa zinazouzwa na nchi mbalimbali kama vile korosho, kahawa, pamba na parachichi.

Pia, kuhusu suala la nishati, TanTrade imeweza kushirikiana na Kenya katika usambazaji wa nishati ya kisasa na iliyo salama na itaendelea kujumuisha nchi mbalimbali ilikukuza soko la nishati vilevile,katika mdahalo amewashauri wajasiliamali kuhusu ufanyaji wa utafiti kabla ya kuleta bidhaa sokoni kwani itasaidia katika kutambua mahitaji ya wateja na kupata njia mbalimbali za kuwa hudumia.

TANTRADE YAENDELEA KUTOA FURSA ZA “INTERNSHIP” KWA WANAFUNZI WA VYUO MBALIMBALI HAPA NCHINI.

 

Mikutano ya Usalama wa Chakula Africa(AGRF 2023).

 

TANTRADE YAWAJENGEA UWEZO WANAFUNZI WA MASOMO YA BIASHARA NCHINI ILI WAZIJUE SHERIA, KANUNI NA TARATIBU ZA UFANYAJI BIASHARA ZILIZOWEKWA NA SERIKALI.


.................................
 TanTrade Dar es salaam.
 18 Agusti 2023.

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Leo Tarehe 18 Agusti 2023, imetoa Mafunzo  kwa Wanafunzi wa kidato cha tano wa shule ya Sekondari BaoBab iliyopo jijini Dar es salaam, yenye  malengo ya kujua kazi za TanTrade na kuwajengea uwezo Wanafunzi hao ili kuelewa ni kwa namna gani TanTrade  inafanya kazi ili kuwasaidia Jumuiya ya Wafanyabiashara, pamoja na kufahamu miongozo mbalimbali ya Ufanyajibiashara nchini.

 
Mafunzo hayo yamefanyika Leo Tarehe 18 Agusti 2023 katika ukumbi wa TanTrade uliopo barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam.


Akitoa mada katika Mafunzo hayo Afisa Biashara kutoka TanTrade Bi. Marcelina Antony amesema TanTrade ni Taasisi ya Serikali iliyopewa Mamlaka ya udhibiti, utendaji,  na ushauri wa kuendeleza na kukuza biashara za ndani na nje ya Tanzania.
Hivyo Wafanyabiashara wengi wamenufaika kupitia TanTrade kwa kujengewa uwezo wa kuwezeshwa kufanya biashara kiutaalamu na kiushindani kupitia Mafunzo ya Biashara.

Pia TanTrade imefanikiwa kuwaunganisha wafanyabiashara kutoka Tanzania na wauzaji na wanunuzi kutoka nje ya nchi, na kuwasaidia  Wafanyabiashara kukua kibiashara kupitia Maonesho ya biashara yanayoratibiwa na TanTrade kama vile , Maonesho ya SabaSaba pamoja  na misafara mbalimbali ya biashara.

Naye Afisa Biashara kutoka TanTrade Bi.  Mwanaidi Chiro ameongeza kuwa  TanTrade pia inahusika na  Wafanyabiashara wanaofuata sheria za nchi za Ufanyaji biashara  na inaandaa  Makongamano mbalimbali ya kibiashara, kwa mfano  kongamano la sudani  ambapo tulipata oda ya Mahindi na tulitangaza huduma zetu  za afya kama vile huduma zinazotolewa na hospitali ya  Muhimbili, Kwa kufanya hivyo  tulitangaza bidhaa na  huduma zinazozalishwa na Watanzania na kusaidia  Wafanyabiashara  kupata Masoko makubwa ya nje ya nchi. 

Sambamba na hayo TanTrade pia ina jukumu la kuratibu misafara na Makongamano mbalimbali ya ndani na nje ya Tanzania.


"Kama kuna Waoneshaji wanatoka nje ya nchi na  kuja Tanzania kuonesha bidhaa zao, wanakaguliwa kama wamekidhi vigezo na kufuata sheria za uoneshaji ikiwa ni pamoja na kuomba  vibali na kukamilisha  taratibu zote.  hivyo Serikali inahusika na  utengenezaji wa  Mazingira wezeshi ya kufanya biashara, ikiwa ni  pamoja na kutengeza mifumo wezeshi na rafiki ili kuhakikisha kwamba muuzaji anaweza kuuza na kununua biashara.’’ Alisema.



Aidha Afisa Biashara kutoka TanTrade Bw. Melchizedek Salingo aliongeza kuwa TanTrade inawasaidia Wafanyabiashara kwa   kufanya utafiti wa Soko la ndani na Soko la nje ili kujua ni bidhaa zipi zinazohitajika sokoni ili Wafanyabiashara waweze kuzalisha na kutoa huduma inayotokana na mahitaji ya Soko husika.

Naye Mwalimu wa somo la Biashara kutoka shule ya sekondari ya BaoBab Mwl. Mtinda kengela kwa niaba ya shule ya BaoBab ametoa shukrani kwa Uongozi wa TanTrade kwa kuwapokea na kuwapa mafunzo Wanafunzi hao  yatakayowajenga kibiashara.

TANTRADE YASHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WATENDAJI WAKUU WA TAASIS ZA UMMA.


TANTRADE YASHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WATENDAJI WAKUU WA TAASIS ZA UMMA.

Mamlaka ya Maendeleo ya biashara Tanzania (TanTrade) ikiwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Bi. Latifa Khamis imeshiriki katika Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kilichofanyika Agosti 19, 2023 Jijini Arusha.

Katika Kikao hicho cha Kazi
Mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amewasisitiza Watendaji Wakuu wa Taasisi hiyo kuweka Uzalendo mbele katika kutekeleza majukumu yao na kuwa sehemu ya mabadiliko chanya.
Pia amewataka kuwa tayari kwa mageuzi katika Taasisi za Umma kwa Maendeleo ya Taifa

Pia alieleza kuwa kutakuwa na ushirikiano wa kutosha kutoka Serikalini ili kufikia malengo na kuleta tija kwa Taasisi hiyo.

August 28, 2023

 

TANTRADE WAUNGANISHA KAMPUNI ZA TANZANIA NA KAMPUNI YA MAGNIT KUTOKA URUSI 30 AGOSTI 2023

 

28 AGOSTI 2023 DAR ES SALAAM