TANTRADE YASHIRIKI MKUTANO WA MAANDALIZI YA EXPO 2023 DOHA


10 Septemba, 2023.

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeshiriki mkutano wa mwisho wa maandalizi ya Expo 2023 Doha unaofanyika tarehe 10-11 Septemba, 2023, Doha, Qatar.

Mkutano huo umeshirikisha Makamishna wakuu wa Nchi 56 Duniani zinazoshiriki Maonesho ya Kilimo cha Mboga Mboga yanayojulikana kama Doha Horticultural Expo ukiwa ni muendelezo wa matayarisho hayo ambapo Timu ya Expo iliwasilisha hatua za matayarisho kwa makamishna hao ili kurahisisha ushiriki wao katika maonesho yanayotarajiwa kuanza tarehe 2 Octoba, 2023 hadi 28 Machi 2024.
Kwa upande wa Tanzania, mkutano umewakilishwa na Bw.Tahir M.Ahmed na Bi. Mwanaidi K. Chilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa Banda la Tanzania, Bi. Latifa M. Khamis, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade.

TANTRADE KUSHIRIKI KATIKA UFUNGUZI WA MAFUNZO YA UJASILIAMALI KWA WANAWAKE


DAR ES SALAAM.
12 SEPTEMBA, 2023

Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania (TanTrade) kushiriki na wafanyabiashara katika  ufunguzi wa mafunzo na kufanya mdahalo kuhusu   Ujasiliamali katika ukumbi wa Kibada Garden Kigamboni- Dar es salaam tarehe 12 Septemba, 2023.

Ambapo, Afisa wa TanTrade Bi.Lulu Masanje amesema Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania inatoa mafunzo juu ya kujikwamua kibiashara ndani na nje ya nchi ambapo jukumu la kwanza ni kutoa taarifa mbalimbali za biashara ambazo zinampa fursa mfanyabiashara kufahamu kuhusu takwimu ambazo  bidhaa zinauzwa sana na kuongeza soko kwa wingi zaidi na itamsaidia mfanyabiashara kufanya maamuzi sahihi kwaajili ya kujikwamua kiuchumi.

Vilevile, TanTrade inatoa fursa za masoko, mabanda ya maonyesho na usafirishaji wa bidhaa kwenda nchi mbalimbali ambapo fursa hizi   zitachangia katika kuongeza uchumi binafsi na nchi kwa ujumla. Kadhalika, kutambua takwimu za bidhaa zinazouzwa na nchi mbalimbali kama vile korosho, kahawa, pamba na parachichi.

Pia, kuhusu suala la nishati, TanTrade imeweza kushirikiana na Kenya katika usambazaji wa nishati ya kisasa na iliyo salama na itaendelea kujumuisha nchi mbalimbali ilikukuza soko la nishati vilevile,katika mdahalo amewashauri wajasiliamali kuhusu ufanyaji wa utafiti kabla ya kuleta bidhaa sokoni kwani itasaidia katika kutambua mahitaji ya wateja na kupata njia mbalimbali za kuwa hudumia.

TANTRADE YAENDELEA KUTOA FURSA ZA “INTERNSHIP” KWA WANAFUNZI WA VYUO MBALIMBALI HAPA NCHINI.

 

Mikutano ya Usalama wa Chakula Africa(AGRF 2023).