DAR-ES-SALAAM INTERNATIONAL Trade Fair(DITF)
Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano, TANTRADE wakutana na East Africa Commercial and Logistics Center (EACLC)- Shanghai

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Nyumba Zanzibar Dkt. Mngereza Mzee Miraji wawakilishi wa TanTrade wakiongozwa na Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara Bw. Fortunatus Mhambe na mwakilishi kutoka Kampuni ya Kahawa ya Africafe Bw. Abdulhakim Mulla walikutana katika ofisi kuu ya EACLC iliyopo Shanghai-China kwa ajili ya kusikiliza wasilisho kutoka kwa Lisa Wang ambaye ni Mwenyekiti wa EACLC ambaye katika wasilisho lake alishukuru Serikali ya Tanzania kuendelea kuipa fursa ya kiuwekezaji kampuni yake ya EACLC.
Lisa alitumia wasaa huo kuorodhesha miradi ambayo kampuni yake inaendelea na utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na
- Mradi Mkubwa wa Soko Kuu La Kimataifa la Afrika Mashariki -Ubungo Dar Es Salaam linaloendelea na ujenzi wake ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024 ambao utakuwa na maduka zaidi ya 2,000 na kufanya Jiji la Dar Es Salaam kupokea wageni kutoka takribani nchi 9 ambazo zitakuwa zikinunua bidhaa hapo badala ya kusafiri mpaka nchini China.
- Mradi wa Ujenzi wa Hospitali Zanzibar na
- Mradi wa Maghala ya Uhifadhi wa Bidhaa zitakazouzwa nje ya nchi na zitakazoletwa nchini Tanzania utaokuwa maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Zanzibar
Vilevile Lisa Wang aliongeza kwa kuishukuru TanTrade kwa kuendelea kuiunga mkono kampuni ya EACLC na kusema kuwa kutokana na ushiriki wao mzuri katika Maonesho ya Sabasaba {DITF} ya 47 ya 2023 wafanyabiasha wengi zaidi kutoka China wameonesha nia ya kushiriki katika Maonesho yajayo ya 48 ya DITF, 2024.
Aidha, Bi. Lisa Wang ameahidi kuendelea kuitangaza Tanzania ikiwamo kushiriki katika Maonesho yatakayofanyika Januari, 2024 Zanzibar.
Kwa upande wake Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China alimwakikishia Lisa Wang kuwa Serikali inatambua Mchango Mkubwa EACLC inafanya kwa nchi ya Tanzania na kuwa wataendelea kumpa ushirikiano.
Naye Bw. Fortunatus Mhambe ambaye ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara alimpongeza Lisa kwa kuleta washiriki wa Maonesho ya Sabasaba kutoka China wapatao 187. Aidha, alimpongeza Lisa kwa kampuni yake kudhamini Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar Es Salaam ya 2023
Lisa alitumia wasaa huo kuorodhesha miradi ambayo kampuni yake inaendelea na utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na
- Mradi Mkubwa wa Soko Kuu La Kimataifa la Afrika Mashariki -Ubungo Dar Es Salaam linaloendelea na ujenzi wake ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024 ambao utakuwa na maduka zaidi ya 2,000 na kufanya Jiji la Dar Es Salaam kupokea wageni kutoka takribani nchi 9 ambazo zitakuwa zikinunua bidhaa hapo badala ya kusafiri mpaka nchini China.
- Mradi wa Ujenzi wa Hospitali Zanzibar na
- Mradi wa Maghala ya Uhifadhi wa Bidhaa zitakazouzwa nje ya nchi na zitakazoletwa nchini Tanzania utaokuwa maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Zanzibar
Vilevile Lisa Wang aliongeza kwa kuishukuru TanTrade kwa kuendelea kuiunga mkono kampuni ya EACLC na kusema kuwa kutokana na ushiriki wao mzuri katika Maonesho ya Sabasaba {DITF} ya 47 ya 2023 wafanyabiasha wengi zaidi kutoka China wameonesha nia ya kushiriki katika Maonesho yajayo ya 48 ya DITF, 2024.
Aidha, Bi. Lisa Wang ameahidi kuendelea kuitangaza Tanzania ikiwamo kushiriki katika Maonesho yatakayofanyika Januari, 2024 Zanzibar.
Kwa upande wake Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China alimwakikishia Lisa Wang kuwa Serikali inatambua Mchango Mkubwa EACLC inafanya kwa nchi ya Tanzania na kuwa wataendelea kumpa ushirikiano.
Naye Bw. Fortunatus Mhambe ambaye ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara alimpongeza Lisa kwa kuleta washiriki wa Maonesho ya Sabasaba kutoka China wapatao 187. Aidha, alimpongeza Lisa kwa kampuni yake kudhamini Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar Es Salaam ya 2023
Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Sita ya Bidhaa na Huduma (6th International Import Expo -CIIE ) ya Shanghai - China ambayo yameanza tarehe 5 hadi 10 Novemba, 2023

Maonesho hayo ambayo yanatoa fursa kwa nchi mbalimbali kuuza bidhaa nchini China yalifunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa China Mheshimiwa Li Qiang.
Katika Maonesho haya nchi zaidi ya 127 zinashiriki zenye zaidi ya Waoneshaji 2800. Aidhaa bidhaa mbalimbali za Kilimo, Mazao Teknolojia na Ubunifu mpya 438 zenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 73.52 zinaoneshwa.
Katika Maonesho haya kutakuwa na mikutano 24 ya kibiashara na uwekezaji ambayo itahudhuriwa na Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi za Biashara na Uwekezaji na Sekta Binafsi wakikutanishwa na taasisi mbalimbali na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa wakiwemo ITC, WTO UNDP na UNIDO.
Aidha, katika mikutano hiyo fursa mbalimbali za kibiashara na uwekezaji zitajadiliwa kwa undani.
Maonesho haya ya 6 ya Huduma na Bidhaa ya China (CIIE) ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara watanzania kuonesha Bidhaa na Huduma zao kwa jamii ya China na kuweza kuwaunganisha na masoko ili kukuza mitaji yao na kukuza uchumi wa Taifa kiujumla.
Msafara wa washiriki kutoka Tanzania katika Maonesho haya waliongozwa na Maafisa kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) chini ya Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara, Bw. Fortunatus Mhambe. Washiriki katika Maonesho haya kutoka Tanzania ni pamoja na ZAFICO, PBZ, TRA, ZBS, Africafe na KMVL.
Aidha, TANTRADE imesimamia ushiriki wa baadhi ya makampuni na taasisi ambazo zimewasilishwa sampo bila ushiriki wao binafsi ikiwamo kampuni Ya AMIMZA inayouza kahawa nje ya nchi.
Katika Maonesho haya nchi zaidi ya 127 zinashiriki zenye zaidi ya Waoneshaji 2800. Aidhaa bidhaa mbalimbali za Kilimo, Mazao Teknolojia na Ubunifu mpya 438 zenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 73.52 zinaoneshwa.
Katika Maonesho haya kutakuwa na mikutano 24 ya kibiashara na uwekezaji ambayo itahudhuriwa na Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi za Biashara na Uwekezaji na Sekta Binafsi wakikutanishwa na taasisi mbalimbali na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa wakiwemo ITC, WTO UNDP na UNIDO.
Aidha, katika mikutano hiyo fursa mbalimbali za kibiashara na uwekezaji zitajadiliwa kwa undani.
Maonesho haya ya 6 ya Huduma na Bidhaa ya China (CIIE) ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara watanzania kuonesha Bidhaa na Huduma zao kwa jamii ya China na kuweza kuwaunganisha na masoko ili kukuza mitaji yao na kukuza uchumi wa Taifa kiujumla.
Msafara wa washiriki kutoka Tanzania katika Maonesho haya waliongozwa na Maafisa kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) chini ya Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara, Bw. Fortunatus Mhambe. Washiriki katika Maonesho haya kutoka Tanzania ni pamoja na ZAFICO, PBZ, TRA, ZBS, Africafe na KMVL.
Aidha, TANTRADE imesimamia ushiriki wa baadhi ya makampuni na taasisi ambazo zimewasilishwa sampo bila ushiriki wao binafsi ikiwamo kampuni Ya AMIMZA inayouza kahawa nje ya nchi.
WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI YA TANTRADE WAPATA SEMINA YA UONGOZI
Tarehe 20 Oktoba, 2023.
DAR ES SALAAM
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) wamepata semina ya Uongozi iliyotolewa na Taasisi ya Uongozi Institute kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina kuanzia tarehe 19 - 20 Oktoba, 2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa TanTrade Jijini Dar es Salaam.
Semina hiyo ya siku mbili ilihusisha mada zikiwemo Uendeshaji wa Shirika na Uongozi Bora, Kufikia Ufanisi wa Bodi, Usimamizi wa Vihatarishi na Msingi wa Udhibiti wa Ndani pamoja na Usimamizi wa Fedha.
DAR ES SALAAM
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) wamepata semina ya Uongozi iliyotolewa na Taasisi ya Uongozi Institute kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina kuanzia tarehe 19 - 20 Oktoba, 2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa TanTrade Jijini Dar es Salaam.
Semina hiyo ya siku mbili ilihusisha mada zikiwemo Uendeshaji wa Shirika na Uongozi Bora, Kufikia Ufanisi wa Bodi, Usimamizi wa Vihatarishi na Msingi wa Udhibiti wa Ndani pamoja na Usimamizi wa Fedha.
Akiongea katika Kufungua rasmi semina hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya TanTrade, Prof. Ulingeta Obadia Mbamba alieleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wajumbe wa Bodi ambapo yanatarijiwa kuongeza Ufanisi zaidi kwenye Utendaji wa Bodi na kuongeza tija kwenye utekelezaji na Usimamizi wa majukumu waliyonayo kama Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka.
TANTRADE YAPATIWA UTAALAM WA KUENDELEZA BIASHARA MTANDAO NCHINI CHINA

Hangzhou, Zhejiang
China
3 Novemba 2023.
Kwa kutambua majukumu ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) ambapo hutekelezwa sambamba na utekelezaji wa
Ilani ya Chama Tawala, Chama cha Mapinduzi( CCM) kilitoa fursa kwa TanTrade kupata mafunzo kwa ajili ya kozi ya E-commerce nchini China. Ufadhili huo ulikuwa chini ya Wizara ya Biashara ya China unaotokana na uhusiano mzuri uliopo katika nyanja mbalimbali kati ya nchi hizo mbili.
Katika kozi hii, watendaji wanne, kutoka CCM (2), TanTrade(1) na DART(1) walioteuliwa kupata mafunzo mahususi kuhusu
Biashara ya mtandao (E-commerce) kuanzia Oktoba 13 hadi Novemba 3, 2023. Mafunzo haya yaliyofanyika katika mji mkuu wa Teknolojia wa Hangzhou, Jimbo la Zhejiang (wakazi milioni 160) yaliendeshwa na Bodi ya Maendeleo ya Biashara Huria ya Zhejiang(ZFTDB) kwa ufadhili wa Wizara ya Biashara - China.
Washiriki wengine muhimu waliotoka nchi zinazoendelea ni pamoja na Sierra Leone, Oman, Pakistan, Cameroon, Nigeria na Mongolia.
Utaalam huu unatolewa wakati biashara za mtandaoni zinaonekana kushika kasi duniani, hasa baada ya janga la COVID-19 ambapo wafanyabiashara wanatumia mifumo ya kisasa ya mtandao, akili bandia (AI) na mitandao ya kijamii katika kutafuta masoko, bidhaa na wateja na pia kuuza kwa njia za moja kwa moja ni kupitia Utiririshaji wa moja kwa moja wa video.
Wataalam wamepata maarifa mengi juu ya jinsi ya kuunganisha uchumi wa kidijitali, biashara ya mtandaoni na ukuaji wa miji na utalii, mbinu za masoko ya mtandao na bei, uundaji wa vituo vya biashara na miundombinu wezeshi, mauzo na manunuzi kwenye mtandao na kuona kwa wenyewe jinsi masoko ya miji muhimu ya Hangzhouh (teknolojia), Zhuji (vito), Putian (viatu) na Tongxian (mavazi) iliyoko Zhejiang China yanavyofanya kazi kwa ufanisi.
Vile vile, wataalam waliotembelea na kusikiliza mihadhara iliyotolewa na makampuni yanayoongoza katika biashara ya mtandaoni ya mpakani ikijumuisha Alibaba Group, Dahua Technologies, SunHigh na Wensli Silk na Chinagoods.com; ambapo biashara za mtandaoni huchangia zaidi ya asilimia 30 katika mapato ya Jiji la Zhejiang na kuchangia wastani wa yuan bilioni 279 kwa mwaka.
Wataalamu hao wameishukuru Serikali na vyama hivyo kwa kuendelea kukuza Diplomasia ya Uchumi na Biashara na kuahidi kutumia elimu waliyoipata kulitumikia Taifa katika kukuza Biashara na uchumi kwa kuendelea kuwajengea uwezo na ushauri kwa watendaji, Taasisi na wajasiriamali.
------------------------------------
Picha: Tuzo za vyeti kwa maafisa wanne wa Kitanzania na wahitimu wenzao.
China
3 Novemba 2023.
Kwa kutambua majukumu ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) ambapo hutekelezwa sambamba na utekelezaji wa
Ilani ya Chama Tawala, Chama cha Mapinduzi( CCM) kilitoa fursa kwa TanTrade kupata mafunzo kwa ajili ya kozi ya E-commerce nchini China. Ufadhili huo ulikuwa chini ya Wizara ya Biashara ya China unaotokana na uhusiano mzuri uliopo katika nyanja mbalimbali kati ya nchi hizo mbili.
Katika kozi hii, watendaji wanne, kutoka CCM (2), TanTrade(1) na DART(1) walioteuliwa kupata mafunzo mahususi kuhusu
Biashara ya mtandao (E-commerce) kuanzia Oktoba 13 hadi Novemba 3, 2023. Mafunzo haya yaliyofanyika katika mji mkuu wa Teknolojia wa Hangzhou, Jimbo la Zhejiang (wakazi milioni 160) yaliendeshwa na Bodi ya Maendeleo ya Biashara Huria ya Zhejiang(ZFTDB) kwa ufadhili wa Wizara ya Biashara - China.
Washiriki wengine muhimu waliotoka nchi zinazoendelea ni pamoja na Sierra Leone, Oman, Pakistan, Cameroon, Nigeria na Mongolia.
Utaalam huu unatolewa wakati biashara za mtandaoni zinaonekana kushika kasi duniani, hasa baada ya janga la COVID-19 ambapo wafanyabiashara wanatumia mifumo ya kisasa ya mtandao, akili bandia (AI) na mitandao ya kijamii katika kutafuta masoko, bidhaa na wateja na pia kuuza kwa njia za moja kwa moja ni kupitia Utiririshaji wa moja kwa moja wa video.
Wataalam wamepata maarifa mengi juu ya jinsi ya kuunganisha uchumi wa kidijitali, biashara ya mtandaoni na ukuaji wa miji na utalii, mbinu za masoko ya mtandao na bei, uundaji wa vituo vya biashara na miundombinu wezeshi, mauzo na manunuzi kwenye mtandao na kuona kwa wenyewe jinsi masoko ya miji muhimu ya Hangzhouh (teknolojia), Zhuji (vito), Putian (viatu) na Tongxian (mavazi) iliyoko Zhejiang China yanavyofanya kazi kwa ufanisi.
Vile vile, wataalam waliotembelea na kusikiliza mihadhara iliyotolewa na makampuni yanayoongoza katika biashara ya mtandaoni ya mpakani ikijumuisha Alibaba Group, Dahua Technologies, SunHigh na Wensli Silk na Chinagoods.com; ambapo biashara za mtandaoni huchangia zaidi ya asilimia 30 katika mapato ya Jiji la Zhejiang na kuchangia wastani wa yuan bilioni 279 kwa mwaka.
Wataalamu hao wameishukuru Serikali na vyama hivyo kwa kuendelea kukuza Diplomasia ya Uchumi na Biashara na kuahidi kutumia elimu waliyoipata kulitumikia Taifa katika kukuza Biashara na uchumi kwa kuendelea kuwajengea uwezo na ushauri kwa watendaji, Taasisi na wajasiriamali.
------------------------------------
Picha: Tuzo za vyeti kwa maafisa wanne wa Kitanzania na wahitimu wenzao.
Subscribe to:
Comments (Atom)
-
Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Taasisi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) tarehe 10 Agosti hadi 12 Agosti 2023,i...
